Katibu mkuu wa umoja wa mataifa Antonio Guterres amesema hatua ya rais Trump kuutambua mji wa Jerusalem kama makao makuu ya Israel inaleta wasi wasi katika jitihada za kuleta amani katika mzozo wa Israel na Palestina.

Akizungumza na CNN Guterres ametoa msimamo huo siku ambayo pia msemaji wa makamu wa rais wa Marekani Mike Pence ameishutumu serikali ya Palestina.

Msemaji huyo ameongeza hakufurahiswa na kitendo cha rais wa Palestina Mahmoud Abbas kushindwa kukutana na kiongozi huyo wa Marekani kwa sababu ya mzozo wa mji wa Jerusalem.

Waandamanaji wameendelea kukusanyika mitaani katika nchi za Kiaarabu wakipinga hatua hiyo ya raia Trump.

Naye Papa Francis ambaye ni kiongozi wa kidini wa wakatoliki wapatao billion moja duniani ametoa maoni yake,akisema kuwa Jerusalem ni mji mtakatifu kwa wakristo,Wayahudi na Waislam.

Amesema ni mazungumzo pekee yanayoweza kuleta suluhu katika mzozo huo wa Irael na Palestina.

SOMA ZAIDI