TRA kupiga mnada jengo la Star TV
KAMPUNI ya Sahara Media Group (SMG), inayomiliki kituo cha Televisheni Star tv, Redio Free Africa (RFA) na Kiss FM imefungwa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kushindwa kulipa kodi ya Sh. 4.5 bilioni, anaandika Irene Emmanuel.
Pia kampuni hiyo imepewa siku 14 (wiki mbili) kuanzia sasa, iwe imelipa kiasi hicho cha fedha na kama haitafanya hivyo majengo ya kampuni hiyo yatapigwa mnada ili kufidia deni hilo.
Kampuni hiyo inayomilikiwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, Anthony Diallo, inadaiwa kiasi hicho cha fedha za malimbikizo ya kodi ya kipindi cha awali huku kipindi cha miaka miwili 2016 – 2017 bado akiwa anadaiwa fedha ambazo hazijawekwa wazi.
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni ya Sukar Action Mart na Court Brokers, Lyasuka Sarehe, amesema kuwa wamechukua hatua hiyo baada ya kampuni hiyo kushindwa kulipa kiasi hicho cha fedha.
Salehe amesema kuwa kutokana na hali hiyo, wanachukua ya kuifunga huku wakitoa siku 14 kuanzia sasa, fedha hizo ziwe zimelipwa na kwamba kama haitafanya hivyo, watachukua hatua nyingine yakupiga mnada jengo hilo.
“Hizi siku 14 tulizotoa akishindwa kulipa tutaitisha mnada wa hadhara kwa ajili ya kukomboa kodi ya Serikali na kama kampuni isipolipa tutapiga mnada jengo hilo,” amesema Sarehe.
Anthony Diallo, Mmiliki wa Sahara Media ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, |
Post a Comment