Mawakala wa mitandao ya simu wazungumzia adha wanayo pata wakati wa kusajili laini za simu
Duka linalo husika na kutoa huduma ya mitandao ya simu hapa iliyoko morombo jijini Aruha. |
Akizungumza na mwandishi wa habari hii moja wa wakala wa kampuni ya vodacom wamezungumzia changamoto mbalimbali kuwa ni pamoja na baadhi ya wateja kutokuja na vitambulisho pindi wanapo kuja kusajili laini zao.
aidha wameiomba serkali kuweka sheria kali ili waweze kuondokana na adha hiyo kwani baadhi ya wateja wao wamekuwa hawaji na vitambulisho halali jambo linalo adhiri huduma zao kutofanya vizuri.
wakala wa mtandao ya vodacom akitoa huduma kwa mteja |
Pia wametoa wito kwa watumiaji wa simu za mkononi na mitandao ya simu kuepuka kutumia vitambulisho ambavyo siyo ya kwao kwani ni kosa kisheria.
Aidha kwa upande wa watumiaji wa mitandao hiyo wamekiri kuwepo kwa tatizo hilo la baadhi ya wateja kutumia vitambulisho feki pindi wanapo sajili laini zao kwani wananchi wengi hawana elimu kuhusu usajili wa laini jambo linalo pelekea watu kutumia vitambulisho ambayo siyo vya kwao.
www.dailhabaritz.blogspot.com
Post a Comment