Qatar kudai fidia kutoka nchi zilizoitenga
Mji mkuu wa Qatar Doha |
Nchi ya Ghuba ya Qatar imesema itadai fidia dhidi ya nchi zake jirani zilizoitenga nchi hiyo hasa kiuchumi.
Nchi za Saudi Arabia, UAE, Bahrain na Misri zote zimekata mahusiano ya anga, ardhi na bahari na Qatar baada ya kuishutumu kuunga mkono makundi ya kigaidi.
- Qatar yakataa kuafikia masharti iliowekewa
- India kuwasafirisha raia wake kutoka Qatar
- Madhara yatakayoletwa na kuitenga Qatar
- Qatar yanunua ndege za kivita kutoka Marekani
Qatar imekana madai hayo, na imeunda tume itakayoshughulikia malalamiko ya hasara iliyopatikana kwa kampuni zake pamoja na watu binafsi.
Qatar kudai fidia kutoka nchi zilizoitenga |
Walalamikaji hao wanaweza kuwemo shirika la ndege la taifa, ambalo limebidi kubadili njia licha ya awali kutumia anga za nchi jirani.
Post a Comment